Siku iliyofuatia Rais wa Marekani, Barack Obama aliguswa, akaandika kwenye ukurasa wake Facebook kwamba anamkaribisha ndani ya Ikulu ya Marekani kama njia ya kufanya watoto wapende somo la Sayansi.
Ahmed alikuwa mwanafunzi wa Shule ya MacArthur High School iliyoko Irving, Texas Marekani… kingine kuhusu yeye leo ni kwamba Baba wa Ahmed, Mohamed Elhassan Mohamed amethibitisha kwamba Familia haiko tayari kumrudisha Ahmed Shuleni hapo.
Japo Polisi waliridhika na Uchunguzi kwamba kifaa alichokamatwa nacho sio Bomu, msimamo wa Shule uko palepale… wanasema hairuhusiwi mwanafunzi kuja na vitu ambavyo vimekatazwa Shuleni hapo, kwa hiyo hata hiyo ya Ahmed kukamatwa hawako tayari kuomba radhi.
;