Juma Nature adai mshindani wake kwenye muziki kwa sasa ni Diamond


 Msanii mkongwe wa muziki, Juma Nature amedai msanii pekee ambaye anaweza akashindana naye kwa sasa ni Diamond.
Akizungumza na tovuti ya Times Fm, Juma Nature ameomba wadau kuandaa tamasha ili washindanishwe.
“Watu wanamtukuza sawa lakini watuweke stage moja tuone nani atakamua, unajua tuseme ukweli bongo flava sasa mimi na Diamond ndio wapinzani pekee,” alisema Juma Nature.
Aliongeza, “Watu waandae pambano, na mpunga pia uwepo nioneshe na mimi nguvu yangu ilivyo mtaani,”
Nature amesema anaamini muziki wake aliyokuwa anafanya zamani una nguvu kubwa kuliko huu wa wasanii wa sasa.


x

;

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »