Yanga,Mazembe watupwa nje michuano ya klabu bingwa Africa


Wawakilishi wengine wa Tanzania katika michuano ya Afrika wakicheza Ugenini huko Nchini Misri, Yanga wamefungwa 2-1 na Al Ahly na kuondolewa katika michuano ya klabu bingwa Africa.
Mabingwa watetezi Tp Mazembe wakaondolewa katika michuano hiyo baada ya sare ya 1-1 dhidi Wydad de Casablanca, na Casablanca wakisonga mbele kwa ushindi 3-1.
Enyimba wakasonga mbele kwa ushindi wa penati 4-3 dhidi ya Etoile du Sahel ,As Vita Club nao wakasonga mbele licha ya kufungwa kwa mabao 2-1 na Mamelod Sundowns .
Al Ahli Tripoli wakawachapa Asec Mimosas kwa mabao 2-1 lakini asec akisonga mbele kwa kwa jumla ya mabao 3-2
Kwa mujibu wa kanuni za CAF, timu zilizotolewa kwenye hatua ya 16 bora ya michuano ya mabingwa Afrika, zinakutana na timu washindi wa wa hatua ya 16 bora kutoka kombe la sirikisho. Kwa maana hiyo, Yanga inaangukia katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika.


x

;

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »