Hii Kali!SHILOLE adai bila Milioni 20 haumpati Kamwe!


Amepanda dau? Msanii wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefunguka kuwa bila mtu kuwa na kiasi cha Sh. Milioni 20 mkononi, hawezi kucheza filamu yake kwa kuwa kwa sasa anaona kama ni kumpotezea muda.

Akipiga na Ijumaa Wikienda, Shilole au Shishi Baby alifunguka kuwa soko la filamu Bongo, linashuka na pia wasanii wanatumia muda mwingi lakini wanapata malipo kidogo tofauti na nguvu pamoja na muda waliotumia.

“Kama mtu akinitaka kwa sasa ili nicheze filamu yake awe na milioni 20 ndiyo nifanye maana ni kitu ambacho kinachukua muda sana halafu malipo yake ni kidogo,” alisema Shilole.

Chanzo:GPL


x

;

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »